MAALIM SEIF SHARIF AMRIPUA TENA Pr. Lipumba
Mgogoro wa uongozi ndani ya CUF unaendelea kukitikisa chama hicho baada ya jana katibu mkuu wake, Maalim Seif Sharif Hamad kusema Profesa Ibrahim Lipumba hana uwezo wa kumfukuza uanachama huku akimwambia, “Sifukuziki.”
Maalim Seif alitoa kauli hiyo jana katika kongamano la kujadili mwenendo wa CUF lililofanyika Tandale jijini Dar es Salaam, kumjibu Profesa Lipumba ambaye ni mwenyekiti wa chama hicho anayetambuliwa na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa.
Kauli ya makamu huyo kwa kwanza wa Rais wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa (SUK) mwaka 2010 hadi 2015, imekuja siku mbili baada ya Profesa Lipumba kusema Maalim Seif atajadiliwa na kamati ya maadili na nidhamu ya chama hicho kwa utovu wa nidhamu na kudhoofisha CUF.
Katika kile kilichoonekana kumjibu Profesa Lipumba, katibu mkuu huyo alisema kamwe hatakwenda kuhojiwa kwenye kamati hiyo aliyodai ni haramu akisema ipo kinyume cha sheria na taratibu za chama hicho.
“Nitabaki kuwa katibu wa chama hiki hadi uchaguzi wa CUF utakapofanyika mwakani. Kamati ya maadili inamwita Seif, Seif yupi? Siwezi kuungana na wasaliti hata siku moja na wasijisumbue,” alisema.
Alidai kwamba kuna mipango inaratibiwa ya kumfukuza katika wadhifa wake ili nafasi hiyo apewe kiongozi mmoja wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ).
“Kiongozi huyo akiwa katibu mkuu, atapata fursa ya kugombea urais wa Zanzibar lakini ninawaeleza kamwe hawawezi kufanikiwa,” alisema Maalim Seif.
Akijibu madai hayo, mkurugenzi wa habari na mawasiliano kwa umma (CUF Lipumba), Abdul Kambaya alisema anachokifanya katibu mkuu huyo ni sawa na kupiga ramli akisema kitendo chake cha kutofika ofisi za chama hicho, sawa na kujifukuza.
“Maalim Seif alishajifukuzisha CUF kwa sababu hafiki ofisini Buguruni. Kwa hiyo hatuwezi kufukuzana na kulumbana na kivuli chetu wenyewe,” alisema.
Katika kongamano hilo, Maalim Seif pia aligusia jinsi Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) ulivyompokea aliyekuwa mgombea urais wa Chadema katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015, Edward Lowassa na kubainisha kuwa Profesa Lipumba alishiriki kumleta, jambo ambalo mara kadhaa msomi huyo amekuwa akilikanusha.
Pia, Maalim Seif alisema hivi karibuni atafanya ziara kisiwani Pemba na kusema anataka kujihakikishia kama kweli Profesa Lipumba ana wafuasi wengi kisiwani humo kama alivyodai baada ya ziara yake mwezi uliopita.
“Ninawataka wanachama wa CUF kuendelea na mshikamano maana haki itapatikana. Mjitokeze kwa wingi katika kesi zinazoendelea mahakamani. Tuamini kuwa haki itatendeka,” alisema Maalim Seif.
Kongamano hilo lilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa CUF (upande wa Maalim Seif), akiwemo mkurugenzi wa uchaguzi, Sheweji Mketo na naibu katibu mkuu, Joran Bashange na madiwani.
Katika kikao cha baraza la uongozi kilichofanyika Machi 22, Profesa Lipumba alidai kuwa Maalim Seif ameidhoofisha CUF kwa kuwakumbatia viongozi wa Chadema na kutotekeleza azimio la Baraza Kuu la kufungua kesi Mahakama Kuu ya Zanzibar kupinga kufutwa kwa matokeo ya uchaguzi wa wawakilishi na madiwani ambao alisema walikabidhiwa hati za ushindi wa majimbo na Shehia zao katika Uchaguzi Mkuu wa 2015.
Sikuwahi kuamini kitu kama hiki kingeweza kunitokea hadi ndoa yangu ilipokaribia kuisha kabisa.
ReplyDeleteMume wangu alibadilika ghafla. Mwanaume ambaye hapo awali alinipenda na kunijali akawa baridi, asiyejali, na mwenye hasira bila sababu. Aliacha kuonyesha nia katika ndoa yetu, akaniepuka kabisa, na hatimaye akaniomba talaka. Nilivunjika moyo kwa sababu nilimpenda mume wangu kwa moyo wangu wote.
Mambo yalizidi kuwa mabaya aliponizuia kila mahali — WhatsApp, Facebook, Instagram — kana kwamba sijawahi kuwepo. Nililia kila usiku nikijiuliza nilifanya nini kibaya.
Siku moja, rafiki wa karibu alinitembelea na kunitambulisha kwa mtu wa kiroho anayeitwa Dkt. Dawn. Kwa kweli, mwanzoni nilikuwa na shaka, lakini niliamua kumweleza kila kitu kwa sababu sikuwa na chochote cha kupoteza.
Dkt. Dawn alinisomea mambo ya kiroho, na nilishtuka. Alifichua siri kuhusu ndoa yangu na maisha yangu binafsi ambayo hakuna mtu aliyejua. Kila kitu alichosema kilikuwa sahihi 100%. Kisha akafichua kwamba mwanamke mwingine alikuwa amemloga mume wangu. Mwanamke huyu alikuwa akimtembelea mara nyingi, na kwa upumbavu niliamini ilikuwa kuhusu kazi tu.
Dkt. Dawn alinisaidia kuvunja uchawi na akafanya ibada yenye nguvu ya kurejesha upendo kwa ndoa yangu.
Kwa mshangao wangu mkubwa, muda mfupi tu baadaye, mume wangu alinifungulia kizuizi mwenyewe na kuanza kunipigia simu na kunitumia ujumbe mwingi, akiniomba nimsamehe na nirudi nyumbani. Mwanzoni nilimpuuza kwa sababu ya maumivu aliyonisababishia, lakini hatimaye alirudi nyumbani akiwa na zawadi na machozi machoni mwake akiomba nafasi nyingine.
Leo, ndoa yetu ni imara zaidi, yenye furaha zaidi, na yenye amani zaidi kuliko hapo awali. Mapenzi kati yetu yanahisi upya kabisa.
Kana kwamba hiyo haitoshi, Dkt. Dawn baadaye alinisaidia na ibada ya ujauzito kwa sababu tulikuwa tumejitahidi kwa miaka mingi kupata watoto. Ndani ya wiki 8, nilipata mimba kiasili, na leo tumebarikiwa na wavulana wawili wazuri wenye afya njema.
Nitaendelea kushukuru milele.
Ukihitaji: Uchawi wa mapenzi wa kuungana tena na mpenzi wako wa zamani
. Usaidizi wa kurejesha ndoa
. Tamaduni za ujauzito za kupata mimba
. Usaidizi wa kiroho kwa kesi za mahakamani au kupona urithi
. Mwongozo na ulinzi wa kiroho
Ninapendekeza sana Dkt. Dawn. Ushuhuda wangu ni wa kweli, na furaha yangu leo ni uthibitisho. WhatsApp yake: +2349046229159. dawnacuna314@gmail.com