MWANAFUNZI ASHAMBULIWA NA WALIMU, ALAZWA HOSPITALI:
Mwanafunzi wa kidato cha sita katika shule ya sekondari Kalangalala iliyopo Halmashauri ya mji Geita Jonathan Mkono anadaiwa kupigwa hadi kupoteza fahamu na mwalimu mkuu pamoja na mwalimu wake wa nidhamu.
Inadaiwa kwamba mwanafunzi huyo alishambuliwa na mwalimu wake wa nidhamu Rauson Lechapia, pamoja na mwalimu mkuu wa shule hiyo Deusdedit Omchamba baada ya kudaiwa kufanya kosa la kuingia bwenini wakati vipindi vya masomo vikiendelea.
Inadaiwa mwalimu wa nidhamu alimshambulia kwa ngumi sehemu mbalimbali za mwili na baada ya mwalimu mkuu kufikishiwa taarifa za mwanafunzi huyo , alianza kumshambulia kwa viboko hadi kuzirai.
Mwanafunzi huyo amelazwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Geita.
Tukio hili limetokea siku nane tu baada ya mwanafunzi Sperius Eladius mwenye umri wa miaka 13 aliyekuwa akisoma shule ya msingi Kibeta iliyopo mkoani Kagera kudaiwa kupigwa hadi kufa na mwalimu wake Sperius
Post a Comment