MWANAFUNZI ASHAMBULIWA NA WALIMU, ALAZWA HOSPITALI:

Mwanafunzi wa kidato cha sita katika shule ya sekondari  Kalangalala iliyopo Halmashauri ya mji Geita Jonathan Mkono  anadaiwa kupigwa hadi kupoteza fahamu na  mwalimu mkuu pamoja na mwalimu wake wa nidhamu.

Inadaiwa kwamba mwanafunzi huyo alishambuliwa na mwalimu wake wa nidhamu Rauson Lechapia, pamoja na mwalimu mkuu wa shule hiyo Deusdedit Omchamba  baada ya kudaiwa kufanya  kosa la kuingia bwenini wakati vipindi vya masomo vikiendelea.

Inadaiwa  mwalimu wa nidhamu alimshambulia kwa ngumi sehemu mbalimbali za mwili na baada ya mwalimu mkuu kufikishiwa taarifa za mwanafunzi huyo , alianza kumshambulia kwa viboko hadi kuzirai.

Mwanafunzi huyo amelazwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Geita.

Tukio hili limetokea siku nane tu baada ya mwanafunzi Sperius Eladius mwenye umri wa miaka  13 aliyekuwa akisoma shule ya msingi Kibeta iliyopo mkoani Kagera kudaiwa kupigwa hadi kufa na mwalimu wake Sperius 

No comments